Tuesday 21 November 2017

Je, Dk.Shika afanya shuting na Dogo janja?

 Kila siku umaarufu wa Dk.Luis Shika unazidi kuongezeka na hata baadhi ya watu na makampuni wameanza kumtumia katika biahara zao, hii ni pamoj na picha zilizoanza kusambaa zikimuonyesha yupo na msanii wa muziki Dogo Janja. 

Kutokana na picha ambazo zimeanza na zinaendelea kusambaa mtandaoni zikimuonyesha Dk.Shika au Mzee wa 900 Itapendeza akiwa katika muonekano wa kipapa na huku akiwa ana kula bata na warembo, jambo linalohisiwa kuwa huwenda kukawa na video mpya ya muziki kutoka kwa msanii Dogo Janja hivyo ametumika kama muhusika mkuu. 

Dk. Luis Shika amejipatia umaarufu kutokana na sakata la kuuzwa kwa nyumba za mfanyabiashara Said Lugumu, ambapo aliingilia katikwa kutaja kiwango kikubwa cha pesa ili aweze kununua nyumba hicho ila cha kushaa baada ya kuibuka mshindi hakuwa na 25% za kumfanya aweze kuwa mmiliki halali wa nyumba hizo na kufanya polisi wamkamate na kumuweka ndani ambapo alitoka baada ya siku kadhaa na kuanza kupata umaarufu mara dufu. 


No comments:

Post a Comment

Note: only a member of this blog may post a comment.

TANGAZO LA NAFASI ZA MASOMO 2019

https://youtu.be/3CLxlkAGSw0